ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 16, 2024

RAIS RUTO KUMTEUWA MAKAMU WA RAIS MPYA IWAPO SENETI ITAIDHINISHA KUBANDULIWA KWA GACHAGUA


Rais William Ruto anatarajiwa kumteua naibu rais mpya iwapo Bunge la Seneti litaendelea na hatua ya kumtimua Rigathi Gachagua. Picha: Rigathi Gachagua/William Ruto.

Kuondolewa kwa Rigathi Gachagua ofisini kutakuwa ni tukio la kihistoria, kwani itakuwa mara ya kwanza kwa naibu rais aliye madarakani kukabiliwa na mashtaka ya kutokuwa na imani naye katika historia ya Kenya. 

Tumaini la mwisho la Gachagua kuokoa wadhifa wake ni nini? Hatima ya Naibu Rais sasa iko mashakani huku Seneti ikitarajiwa kuanza kujadili mashtaka yake Jumatano, Oktoba 16, na uamuzi wa mwisho ukitarajiwa kufanywa Alhamisi jioni, Oktoba 17.

Matokeo ya mchakato wa kuondolewa kwake yanategemea ikiwa theluthi mbili ya maseneta watapiga kura kumuondoa ofisini. 

Akizungumza na NTV, Wakili wa Mahakama Kuu Steve Ogolla alisema kuwa hatima ya Gachagua sasa iko mikononi mwa Seneti, kufuatia mahakama kukataa kusimamisha Seneti kuendelea na mjadala wa mashtaka ya kutokuwa na imani naye. 

"Hii ilikuwa nafasi yake ya mwisho kusimamisha mchakato huu na hakufanikiwa. Ukweli ni kwamba hatima yake sasa iko mikononi mwa Seneti. Lakini, naamini pia amejiandaa kwa Seneti, tumeona amewasilisha majibu yake kwa hoja hiyo," Ogolla alisema. 

Ni nini kitafuata ikiwa Gachagua ataondolewa na Seneti? Kuondolewa kwa Gachagua kutoka ofisini kunaweza kuacha pengo kubwa ndani ya serikali ya Kenya Kwanza, na kumlazimu mkuu wa nchi kuteua naibu rais mpya kufikia Ijumaa, Oktoba 18. "Kinachoweza kutokea baada ya kuondolewa ni kwamba rais anaweza kuteua mrithi wa Gachagua haraka. 

Lakini kifungu cha 149 bado kinahitaji kuwa mgombea huyo apitishwe na Bunge la Kitaifa ndani ya muda wa siku 60, lakini wanaweza kufanya hivyo haraka," Ogolla aliongeza. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.