ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 14, 2024

RAIS SAMIA APOKEA MWENGE WA UHURU KWENYE KILELE CHA MAADHIMISHO MBIO ZA MWENGE WA UHURU MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wakati akihitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge ambazo kitaifa zimefanyika Jijini Mwanza katika Uwanja wa CCM Kirumba tarehe 14 Oktoba, 2024.

 "Nimehitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru pamoja na Wiki ya Vijana hapa mkoani Mwanza. Ninawashukuru wote waliojitokeza kushiriki tukio hili la kihistoria ambapo Mbio za Mwenge wa Uhuru zimefikisha miaka 60."

"Pongezi kwa wote walioshiriki kuukimbiza kwa mwaka huu na kazi nzuri waliyofanya ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo"


"Nimepokea taarifa ya miradi yote iliyotembelewa katika mbio hizi ambayo inakwenda kunufaisha wananchi kwenye kila kona ya nchi yetu. Nimepokea mapendekezo na salamu za wananchi wa maeneo yote ulikopita Mwenge wa Uhuru, na kwa umakini na uharaka tutayafanyia kazi yale yote yaliyoainishwa kwa manufaa ya Taifa letu"

RAIS wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Oktoba 14, 2024 amewaongoza Viongozi na Wananchi mbalimbali kwenye kilele cha mbio za Mwenge zilizoambatana na Wiki ya Vijana na Nyerere Day katika uwanja CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Rais Samia akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Ndugu Godfrey Eliakim Mzava kwenye Kilele cha Maadhimisho Mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
Matukio mbalimbali katika kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.