ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 5, 2025

CCM PWANI HAWANA DOGO WAMPA MAUWA YAKE RAIS DKT.SAMIA KWA HOTUBA YAKE YENYE TIJA KWA TAIFA

 


Na Victor Masangu,Kibaha


Katibu  wa Siasa ,Uenezi  na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Dkt. David  Mramba   amesema ameipongeza kwa dhati hotuba ya Mhe.Rais Dkt.  Samia Suluhu Hassan  aliyoitoa tarehe Disemba  2 mwaka huu alipozungumza  na wazee wa Jiji la Dar es Salaam na kubainisha kuwa  imegusa masuala  muhimu  yanayohusu Taifa  na kutoa dira na  matumaini  makubwa  kwa maslahi ya kuleta maendeleo  kwa  wananchi wa Tanzania.

  Dkt.Mramba amesema hayo leo tarehe 5 Desemba 2025  katika mkutano na Waandishi  wa Habari uliofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya CCM  wa.  Pwani.

" Chama Cha Mapinduzi  Mkoa wa Pwani  kinaunga mkono  kwa kauli moja kama ifuatavyo;kuimarisha  amani ya Muungano, tunaunga  mkono  msisitizo wa Mhe. Rais  juu ya kulinda amani, utulivu na mshikamano wa Taifa letu kwani amani ndiyo  msingi  wa maendeleo  na hotuba yake imeonesha  dhamira  ya dhati  ya kuendeleza maridhiano,umoja na kudumisha  muungano wetu.

Mramba  amesema kuwa katika kuchochea  uchumi na fursa  za maendeleo Chama Cha Màpinduzi  Mkoa wa Pwani  wanapongeza kwa moyo wote  maelekezo  ya Mhe. Rais  kuhusu  kuendeleza  mageuzi  ya kiuchumi ,kukuza utekelezaji, kuimarisha  miundombinu  na kutengeneza ajira kwa wanawake.

"Katika hotuba ya Mhe.Rais  ameweka wazi  kuwa Serikali  inaendelea  kujenga  mazingira  rafiki ya biashara  na kuhakikisha  matunda  ya uchumi  yanawafikia  wananchi wake" amesema Dkt. Mramba.

Aidha Dkt. Mramba amesema kuwa  Mhe.Rais amesema kuwa  atahakikisha anasimamia  utawala bora  na mapambano  dhidi ya rushwa pia  kwamba CCM  Mkoa wa Pwani  wanaunga  mkono kauli ya Mh.Rais ya kuendeleza  vita dhidi ya  rushwa ,ubadhirifu na matumizi mabaya  ya madaraka kauli yake imedhihirisha kuwa Tanzania  inaongozwa  kwa misingi  ya  haki  uwajibikaji na uwazi.

" Chama Cha Mapinduzi  Mkoa wa Pwani  tunapongeza dhamira  njema  ya Serikali  katika  maeneo yafuatayo:
kuimarisha  sekta  ya afya, kuboresha elimu,kutoa wigo mpana  wa upatikanaji wa maji safi, kuhakikisha huduma bora  za kijamii kwa wazee,vijana  na makundi zinapatikana  kwa wakati ,katika kipengele pia ikumbukwe kuwa  hotuba  ya Mhe.Rais  Inaonesha Uongozi  shirikishi  unaoweka mbele utu na ustawi wa Watanzania" amesisitiza  Dkt. Mramba.

Kuhusu ushirikiano  wa ushirikishwaji wa wazee  amesema ,"CCM  Mkoa wa  Pwani tunaunga  mkono kwa  dhati  utayari wa Mhe. Rais  kusikiliza ushauri wa wazee ,kuthamini mchango wao na kutambua  kama nguzo muhimu ya hekima na utulivu  wa taifa letu".

Dkt. Mramba amehitimisha kwa kusemakuwa  CCM Mkoa wa Pwani  wanaunga mkono hotuba ya Mhe. Rais Samia  kwa sababu kuu nne ikiwa ni pamoja na kuweka  mwelekeo  sahihi wa taifa ,inajenga
matumaini  kwa watanzania ,inasisisitiza mshikamano na inaweka  msingi  wa maendeleo  endelevu  kwa vizazi  vya sasa  na vijavyo.

" Sambamba na  na hayo yote ,Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa wa Pwani  tunampongeza  Mhe.Rais Dkt Samia  Suluhu  Hassan  kwa  uongozi wake  mahiri , wenye hekima  na wa kijasiri kwa kuonesha  uzalendo wa kweli  katika  kulipigania  Taifa. 
CCM  Mkoa wa Pwani kwa umoja wetu, tunaahidi, kushirikiana  na  serikali katika  kutekeleza maelekezo  yote  yaliyotolewa  kwa  manufaa na maslahi ya Taifa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment