ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 18, 2025

VIONGOZI CWT TUKUBALI KUBADILIKA - DKT. DOTO BITEKO

“ Tumetoka mbali, zamani familia iliyokuwa maarufu na kuheshimika kijijini ni ile iliyokuwa na taa ya chemli na watu walijipanga kuangalia namna inavyofaidi mwanga, Dunia imebadilika kwa kiwango ambacho leo hii kila nyumba ina umeme na watu wanaona umeme kama hitaji la lazima kwenye maisha yao, Nataka niwaombe walimu wote nchini endeleeni kuishi kwa dunia inayobadilika, fikirini upya kila siku. Viongozi mnatakiwa kuwafikia walimu wote, kuwasikiliza na kuwahudumia ili wapate sababu ya kuwapenda ”. amesema Dkt. Biteko


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema hayo Oktoba 16, 2025 katika Manispaa ya Musoma, Mkoani Mara wakati akifungua Semina ya Viongozi wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kanda ya Ziwa na kanda ya Magharibi iliyoshirikisha viongozi kutoka mikoa minane.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment