
KIKOSI cha Simba SC kimeondoka bila kipa wake namba moja, Mousa ‘Pin Pin’ Camara raia wa Guinea kwenda Eswatini kwa ajili mchezo wa kwanza za Raundi ya Pili Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Nsingizini Hotspurs.
Kuelekea mchezo huo wa Jumapili ya Oktoba 19 Uwanja wa Taifa wa Somhlolo mjini Lobamba — Simba imeondoka na makipa wawili, Yakoub Suleiman na Hussein Abel.
Timu hizo zitarudiana Jumapili nyingine ya Oktoba 26 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam na mshindi wa jumla ataingia hatua ya makundi inayohusisha timu 16.
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment