
KIKOSI cha Yanga kimewasili salama Jijini Lilongwe, Malawi tayari kwa mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Silver Strikers Jumamosi.
Msafara wa Yanga ulioondoka Saa 1:40 mapema asubuhi ya leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam ulifika Lilongwe Saa 4:44 tayari kwa mchezo huo es Oktoba 18 Uwanja wa Taifa wa Bingu Jijini Lilongwe.
Kocha mpya Msaidizi wa Yanga — Mmalawi Patrick Mabedi ni miongoni mwa waliosafiri na timu wiki moja tangu ajiunge na kikosi cha Wananchi kuliongezea nguvu benchi la Ufundi chini ya Kocha Mkuu, Mfaransa Romain Folz.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment