Makabidhiano hayo ambayo yamefanyika leo katika ukumbi wa Nyumbani Hotel mjini Mwanza yalianza kwa maelezo mafupi kutoka kwa meneja mpango wa baraza la Habari Tanzania Bi. Pili Mtambalike ambaye aligusia matatizo yaliyochangia kukwamisha harakati kadhaa za maendeleo ya chama kwa kipindi kilichopita.
Meneja huyo ameyataja matatizo hayo kuwa ni tatizo la fedha kwa wanachama kutolipa ada kwa muda muafaka, waandishi kukosa weledi wa majukumu yao na migongano ya kiuongozi kati ya waandishi na waandishi.
Rais wa Umoja wa klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC) Bwana. Keneth Simbaya amesema kuwa jukumu kubwa walilonalo wanachama ni kujenga umoja endelevu kwa waandishi wa habari nchini kwa kila wanachama kufanya kazi kwa ufanisi na kiwango cha hali ya juu hivyo kuleta taswira ambayo jamii inahitaji kufikia kimaendeleo
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.