ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 24, 2010

POULSEN SAFARINI, KOCHA MSAIDIZI SLYVESTER MASH ATANGAZA KIKOSI KIPYA STARS KITAKACHO KIPIGA MICHUANO YA NILE.

KOCHA msaidizi wa timu ya taifa ya Tanzania (taifa stars) Silvester Marsh kwaniaba ya kocha mkuu wa timu hiyo Jan poulsen (aliye mapumzikoni kwao Norway) amekitaja kikosi cha wachezaji 23 wa timu hiyo kitakachoshiriki michuano ya kombe la Nile basin mashindano yanayotaraji kuanza kutimua vumbi rasmi tarehe 5 january 2011 nchini Misri.Tofauti na wengi tulivyozoea, Tukio hilo limefanyika leo katika eneo la wazi la uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza ambapo kocha huyo msaidizi yuko ziarani kwa ajili ya shughuli maalum huku likishuhudiwa na Viongozi mbalimbali wa soka waandishi wa habari na wapenzi wa soka wa jiji la miamba.

KIKOSI KAMILI NI KAMA IFUATAVYO
GOALKEEPERS:-
1.JUMA KASEJA - SIMBA SC
2.SHAHBAN KADO -MTIBWA FC
3.SAID MOHAMED - MAJIMAJI SC

DEFENDERS:-
4.SHADRACK NSAJIGWA - YOUNG AFRICAN
5.MWASIKA STEPHANO - YOUNG AFRICAN
6.AGREY MORRIS - AZAM FC
7.KELVIN YONDANI - SIMBA SC
8.JUMA NYOSSO - SIMBA SC
9.NADIR HAROUB - YOUNG AFRICAN

MIDFIELDELS:-
10.IDRISSA RAJABU - SOFAPAKA
11.NURDIN BAKARI - YOUNG AFRICAN
12.SHAHBAN NDITI - MTIBWA FC
13.HANRY JOSEPH - NORWAY
14.JABIR AZIZ - AZAM
15.ABDI KASSIM - YOUNG AFRICAN

FOWARD PLAYERS
16.SALUM MACHAKU - MTIBWA FC
17.MRISHO NGASA - AZAM
18.NIZAR KHALFAN - CANADA
19.GODFREY TAITA - KAGERA SUGAR
20.ATHUMAN MACHUPPA - SWEDEN
21.JERRY TEGETE - YOUNG AFRICAN
22.SAID MAULID - ANGOLA
23.ALI AHMED SHIBOLI - SIMBA SC

Kocha huyo msaidizi amesema kuwa mazoezi ya Stars yataanza rasmi siku ya jumatatu ambapo kambi itakuwa uwanja wa karume jijini dar na tarehe 3jan 2011 wataanza safari kuelekea Misri. Tarehe 5jan2011 Stars kufungua na wenyeji. Wachezaji kama Erasto Nyoni, Mohamed Banka na Haruna Shamte hawajaachwa kutokana na viwango vyao kushuka bali ni kutokana na kuwa majeruhi. Kuhusu suala la kuwarejesha kikosini Machupa na Said Maulid Kocha Marsh amesema kuwa uamuzi huo umekuja kutokana na wachezaji hao kujaa uwezo kwa michezo ngazi za kimataifa.

Kocha Marsh Anauhakika na kikosi hicho alichokitaja kuwa cha ushindi akiwa na imani kubwa kuwa kila mchezaji atacheza kwa bidii na hatimaye kulipandisha soka la Tanzania katika viwango vya soka duniani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.