MNYONGE Mtanzania na zigo la Dowans kwa Tanesco katika mtazano wa Katuni.
Miliki wa Dowans, Suleiman Al Adawi ameibua mjadala mzito nchini tangu alipotua na kufanya mkutano na wahariri wa magazeti matano Jumapili iliyopita, akigoma kupigwa picha pia akizuia televisheni na redio, huku akificha sura yake na sauti. Hata hivyo, mbio hizo za Al Adawi kukwepa kamera za waandishi jana ziliishia ukingoni baada ya kunaswa na kamera za gazeti la Mwananchi wakati akikagua mali zake zilizopo Ubungo.
Mpango mkakati wa kumnasa Al Adawi, ulipangwa na kufanikishwa kwa pamoja na duru huru za habari kutoka kwa raia wema ambao, awali walidokeza kuwa bosi huyo wa Dowans angefanya ziara kukagua mitambo ya kampuni hiyo mapema asubuhi. Swali ni kwamba nini kitafuata baada ya hili....
TEHAMA KUBORESHA ELIMU KWA MAFUNZO YA WALIMU
-
TEHAMA ni nyenzo muhimu katika sekta ya elimu, kwa kutambua hilo Serikali
imewezesha mafunzo kwa walimu ili kuongeza maarifa na kuboresha mbinu za
ufundi...
”Rasmi Soko Kuu la Manispaa ya Bukoba lavunjwa”
-
Soko Kuu la Manispaa Bukoba limevunjwa ili kupisha ujenzi wa soko jipya la
kimataifa unaotarajiwa kuanza muda wowote.
Kwa Wakati tofauti wameonekana Wafa...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.