ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 9, 2018

RC MNYETI AAGIZA VIGOGO 5 UCHIMBAJI MADINI KUKAMATWA.


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ameagiza vigogo watano wachimbaji na wanunuzi wa madini ya Tanzanite katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro na jijini Arusha, kukamatwa na  polisi wakidaiwa kufadhili uchimbaji haramu wa madini hayo.

Leo Februari 8, 2018 kamanda wa polisi Mkoa wa Manyara, Augostino Senga amesema vigogo hao wamekamatwa jana jioni na kulazwa Kituo cha Polisi Mirerani.

Amesema wanawashikilia baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kupata taarifa kuwa, vigogo hao wanashiriki kuwadhamini vijana wanaoingia kwa wizi kwenye migodi ya kampuni ya TanzaniteOne yenye ubia wa asilimia 50 kwa 50 na Shirika la Madini la Taifa (Stamico).

Amesema wanachunguza suala hilo na iwapo vigogo hao ambao majina yao tunayo utakamilika, watafikishwa mahakamani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.