ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 10, 2018

WAZIRI KAKUNDA ATOA MAAGIZO MAZITO MTWARA.

 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda, akisisitiza jambo kwa wawakilishi wa vikundi vya wabanguaji wadogo wa korosho (hawapo pichani). Kwenye kikao hicho Waziri Kakunda ameziagiza taasisi mbalimbali za serikali kuhakikisha zinafanya kazi pamoja kuwawezesha wabanguaji wadogo kushiriki zoezi la kubangua korosho zilizonunuliwa na serikali.
 Mwakilishi wa Mandawa AMCOS kutoka Wilaya ya Ruangwa, Selemani Mwigambe, akiwasilisha hoja wakati wa kikao cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji na wawakilishi wa vikundi vidogo vya ubanguaji wa korosho kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi. Kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kilikuwa na lengo la kutambua changamoto za vikundi hivyo ili kuviwezesha kushiriki zoezi la kubangua korosho iliyonunuliwa na serikali.
Baadhi ya wawakilishi wa vikundi vya wabanguaji wadogo wa korosho kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi wakifuatilia kwa makini maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda(hayupo pichani) kwenye kikao chake na wawakilishi hao leo mjini Mtwara.

GSENGOtV

Waziri Kakunda Atoa Maagizo Mazito MtwaraWaziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda ameziagiza taasisimbalimbali   za serikali   zihakikishe  zinashirikiana kwa   pamoja   ili   kutimiza   azma   yaserikali   kuona   wabanguaji   wadogowadogo   wa   korosho  wanashiriki   kwenye  zoezi   lakubangua korosho iliyonunuliwa na serikali. 

Kwenye   kikao   chake   na   wawakilishi   wa   vikundi   mbalimbali   vya   kubangua   koroshokutoka mikoa ya Lindi na Mtwara, Waziri Kakunda amewaagiza Makatibu Wakuu wawizara yake na ile ya Kilimo kwa kushirikiana na Makatibu Tawala  wa   mikoa   hiyomiwili,   wanahakikisha   wabanguaji   wadogo   wanapewa   ushirikiano   kwa   kupatiwakorosho za kubangua kutoka kwenye maeneo yao.

Kuhakikisha ubora wa korosho itakayobanguliwa na vikundi vya wabanguaji wadogoinakidhi viwango vya soko, mheshimiwa Kakunda amelitaka  Shirika la  Mendeleo  yaViwanda Vidogo (SIDO) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele kwa pamoja wafanyeziara za kutembelea vikundi hivyo ili kujua changamoto zinazowakabili. “Jipangenikuwatembelea   kwenye   maeneo   yao   mjiridhishe   na   kuona   teknolojia   wanazotumiamuwasaidie inapobidi ili ubora wa korosho itakayobanguliwa ulindwe na uwe mzuri”amesisitiza Waziri Kakunda. 

Waziri Kakunda pia ameitaka SIDO ihakikishe inavisaidia vikundi hivyo vya ubanguajimikopo  ya   mashine   itakapothibitika  kikundi kina   uwezo  kufanya  kazi  lakini  hakinavitendea kazi.Kuhusu kilio cha wakulima kudhulimiwa korosho wakati wa kupima, Waziri Kakundaameagiza   Wakala   wa   Vipimo   (WMA)   ianze   mara   moja   zoezi   la   kuhakiki   mizanizinazotumiwa   kwenye   maeneo   ya   kukusanya   na   kupima   korosho.   

Waziri   Kakundaamesema,   “Wakala   wa   vipimo   nchini   watembelee   maeneo   yote   yanayofanyaukusanyaji na upimaji wa korosho kwenye mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma na Pwaniwajiridhishe kama vipimo vinavyotumika vinakidhi matakwa ya kisheria”.

Aidha amewataka Makatibu Tawala wa mikoa wahakikishe wanasimamia utekelezajiwa Sheria ya Ardhi namba 4 na 5 ya mwaka 1999 ambayo inazitaka serikali za mitaangazi ya halmashauri kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi kila kijiji. 

Sheriahizo mbili zimetenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kijamii, kidini nakiuchumi. Utekelezaji wa sheria hizo utawanufaisha wabanguaji wadogo kwa kutengamaeneo watakayo kuwa wanafanya kazi zao bila bughudha. 

Kwa upande wao wabanguaji wadogo wamepongeza hatua iliyochokuliwa na serikaliya   kununua   na   kuhakikisha   korosho   zote   zinabanguliwa   nchini.   “Uamuzi   wakushirikisha wabanguaji wadogo ni jambo la kupongezwa sana, hakika Rais Magufuli nikiongozi   wa   wanyonge”   amesema   Bi.   Daria   Erasto,   Mtendaji   Mkuu   wa   Umoja   waWabanguaji Wadogo wa Korosho Tanzania (UWWKT). 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.