ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 18, 2025

KATIBU MKUU UWT AUNGURUMA KWA WANAWAKE IRINGA AWAFUNDA JUU UMOJA KIPINDI CHA UCHAGUZI MKUU

 


NA MWANDISHI WETU,IRINGA


Katibu Mkuu wa umoja wa wanawake (UWT)  Taifa Ndg. Suzan Peter Kunambi (MNEC) amewahimiza wanawake kuweka misingi imara ya kuwa na umoja na mshikamano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu  ambao unatarajiwa kufanyika Octoba 29 mwaka huu.

Katibu huyo ameyasema hayo wakati wa mikutano mbali mbali kwa ajili ya kuweza kuwanadi na kuwaombea kura wagombea wa CCM katika nafasi ya Urais,Ubunge pamoja na udiwani.

"Kitu kikubwa nawaomba wanawake wenzangu wa iringa mjini pamoja na iringa vijijini kuhakikisha mnashikamana kwa pamoja ili tuweze kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaks huu,"amebainisha Katibu huyo.


Aidha Katibu huyo kupitia mikutano hiyo ameweza kupata fursa ya kuwapokea wanachama wapya 7 kutoka  Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Baadhi ya wanachama hao ambao wamejiunga na CCM  wameahidi kuungana na wanachama wa CCM katika kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu wa UWT  Suzan Peter Kunambi amemnadi wagombea wa CCM nafasi ya Udiwani kata ya Migori  Ndg. Fatma Moge, huku akiwaomba wananchi  kumchagua kwa kura nyingi za kishindo  Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia katibu huyo amewaomba wana ccm kumpa ridhaa ya kuwaongoza na kumpa kura nyingi   Ndg.William Lukuvi ambaye ni Mgombea wa Ubunge Jimbo la Isimani  Wilaya ya Iringa Vijijini.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment