ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 19, 2025

KOKA AOMBA RIDHAA YA KUCHAGULIWA NA WANANCHI KATA YA VISIGA ILI KUWALETEA CHACHU YA MAENDELEO

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA  

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kibaha mjini kupitia tiketi ya Chama cha mapinduzi Silvestry Koka amesema kwamba  endapo akipata ridhaa ya kuchaguliwa ataboresha sekta ya elimu na afya kwa wakazi wa kata ya Visiga.


Koka ameyasema hayo wakati wa  mkutano wa  kampeni katika kata ya Visiga uliohudhuliwa na viongozi mbali mbali wa chama pamoja na wananchi.

Koka amesema kwamba endapo akichaguliwa kupata nafasi hiyo atahakikisha anaboresha elimu kwa kutoa madawati elfu 1000 kwa shule za msingi ili lengo ikiwa ni kuongeza kiwango cha ufaulu.

Amebainisha kwamba pia atashirikiana bega kwa bega na serikali katika kujenga shule moja mpya ya msingi ikiwa sambamba na shule moija mpya ya sekondari katika kata ya Visiga.

Kadhalika Koka amebainisha kuwa katika kuwawekea mazingira  mazuri wanafunzi atahakikisha anaboresha miundombinu ya matundu ya vyoo katika baadhi ya shule.

Akizungumzia kuhusiana na  miundombinu ya nishati ya umeme amebainisha atalivalia njuga suala la nishati ya umeme katika baadhi ya mitaa ikiwemo eneo la Zegereni,Saheni na maeneo mengine ya pembezoni.

Kwa upande wake Mgombea Udiwani kata ya Visiga Mohamed Mpaki amesema kwamba atahakikisha anatekeleza  ilani ya chama kwa vitendo katika miradi mbali mbali ya maendeleo.

Naye Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka lengo kubwa ni kuweza kushinda kwa kishindo katika nafasi ya Urais,Ubunge na Udiwani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment