Kipa wa timu mabingwa Taqwa Sekondari Damian Paul(16) na makeke yake langoni.
Fainali ya Airtel Rising Star imefanyika leo jioni kwenye kituo cha mwanza viwanja vya Buswelu Sekondari ambapo leo kulikuwa na michezo miwili, mchezo wa kwanza umeshuhudia Mwanza Sekondari wakiibuka nafasi ya tatu mara baada ya ushindi wa bao 1 dhidi ya Buswelu sekondari goli likipatikana kwa njia ya penati (pichani) mfungaji akiwa ni Selemani Ibrahimu aliyefanikiwa kumhadaa kwa ufundi kipa wa timu pinzani.
Mabingwa Taqwa Sekondari.
Aka Chicharito mchezaji wa Taqwa aliyekuwa mwiba kwa Nsumba.
Nsumba Sekondari.
Mchezo wa pili wa fainali ulikuwa ni kati ya Nsumba Sekondari na Taqwa kipute kilichoanza kwa kasi ya ajabu na ushindani mkubwa lakini hadi dakika za kawaida za mchezo zinamalizika ngoma droo 0-0 ndipo ikaamuliwa njia ya matuta iliipa ushindi Taqwa kwa penati 4-3, penati zilipigwa nane, nane.
KOICA Yajenga Maabara ya Kisasa ya 3D ATC
-
Na Woinde Shizza, Arusha
Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya
Kimataifa la Korea (KOICA), kimezindua rasmi maabara...
Simba SC inafahamu la kufanya ili 'kupindua meza'
-
Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids amesema wachezaji na jopo la ufundi
wanafahamu fika wanachopaswa kukifanya katika mchezo wa marejeano wa
fainali ya Ko...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.