IMEANDIKWA NA. VICTOR MASANGU/PWANI SAUTI NA ALBERT G.SENGO Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Charles Mahera,amewataka walimu, wazazi, pamoja na walezi nchi nzima kuhakikisha kwamba wanaweka mipango madhubuti ambayo itaweza kuwalinda na kuwatunza watoto na wanafunzi kwa lengo ikiwa ni kuweza kupambana na wimbi la vitendo vya unyanyasaji na ukatili ili waweze kusoma katika mazingira ya usalama na amani. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Aprili 29, 2025 wakati wa kufunga rasmi mafunzo ya matumizi bora na salama ya vifaa vya TEHAMA kwa walimu wa shule za msingi, yanayotekelezwa kupitia Mradi wa Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) ambayo yamefanyika katika ukumbi wa shirika la elimu Kibaha Mkoani Pwani na kushirikisha jumla ya walimu wapatao 1,800 kutoka mikoa minne ya Tanzania bara. Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Awali na Msingi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi Suzanne Nusu, amebainisha kwamab kati ya Halmashauri 184 wamejitahidi zimefanikiwa kupata fursa ya kupelekewa vifaa hivyo vya tehama ambapo walimu nao wamenufaika na kupatiwa mafunzo. Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo ya Tehama wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuweza kuona umuhimu wa kuwapa ujuzi wa kuwafundisha teknolojia na kuahidi kwenda kuyafanyia katika kwa weledi katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao katika kuboresha elimu. Mafunzo hayo ya Tehama yameshirikisha walimu wapatao 1800 yamewashirikisha washiriki mbali mbali kutoka Mikoa ya Geita, Tabora,Simiyu pamoja na Kagera ambapo lengo lake ni kuongeza viwango vya sifa za walimu kuanzia elimu ya awali hadi sekondari.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.