ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 5, 2024

SIMBA AU YANGA NANI KULIHESHIMISHA TAIFA HII LEO

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Hizi hapa tambo za mashabiki wa soka toka jijini Mwanza wa timu zilizoishangaza Afrika, Simba na Yanga kwa kuwa timu mbili kutoka taifa moja Tanzana kutinga hatua ya Robo fainali na sasa zikiwa katika safari kuelekea michezo yao ya marudiano kuwania nafasi ya kutinga nusu fainali Klabu Bingwa Barani Afrika. Swali jeh ni nani atakaye liheshimisha Taifa hilo lililopo Afrika Mashariki, ni Simba au Yanga au pengine wababe wote hao? ........................ KWA UPANDE WA UFUNDI. KOCHA Mualgeria wa Simba SC, Abdelhak Benchika amesema kwamba mchezo wa kesho dhidi ya wenyeji, Al Ahly Jijini Cairo utakuwa mgumu, lakini wamejipanga kuwakabili mabingwa wa Afrika. Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari mapema jana Alhamisi Jijini Cairo, Benchika amesema kwamba hawapo Misri kwa ajili ya kufungwa, bali kushindana na hawahofii chochote. Kwa upande wa pili Yanga Africans, kocha wake Muargentina Miguel Angel Gamondi amesema kwamba leo anaweza kumpata mchezaji mmoja tu kati ya wanne aliowakosa kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Waliokosekana kwenye mchezo wa kwanza wa nyumbani ni mabeki Kibwana Shomari, Kouassi Attohoula Yao (Ivory Coast)na viungo Peadoh Pacome Zouazoua (Ivory Coast) na Khalid Aucho (Uganda.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.