ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 1, 2024

WANAOTOROSHA KOROSHO KWENDA NJE YA NCHI WAONYWA, SIKU ZAO ZINAHESABIKA

 

 



Na Oscar Assenga, TANGA.

BODI ya Korosho Tanzania Mkoani Tanga imewaonya wakulima wenye tabia za kutorosha Korosho kwenda kuuza nje ya nchi kuacha mara moja kufanya hivyo kwani siku zao zinahesabika kutokana na vyombo vya dola vinawatambua na watapokamatwa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Moja ya athari za utoroshaji wa Korosho kwenda nje ya nchi ni pamoja na kutokufikia malengo ya uzalishaji ikiwemo nchi mapato ambayo yangeweza kusaidia katika kuchochea maendeleo kwa wananchi wake.

Onyo hilo na Kaimu Meneja wa Bodi ya Korosho Mkoa wa Tanga Atufigwege Mwakyagi wakati akizungumza na waandishi wa habari namna bodi hiyo ilivyojipanga kukabiliana na vitendo hivyo huku wakiwataka wenye tabia hizo kuacha mara moja

Alisema kwani kufanya hivyo maana yake ni kulihujumu zao hilo pamoja na juhudi za Serikali ni kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na bora ili kuweza kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo hicho chenye tija.

“Ndugu zangu mnaotorosha korosho kufanya hivyo ni kosa na vyombo vya dola hivyo tambueni siku zenu zinahesabika sisi kama bodi hatutakubali kuona watu wanahujumu zao hilo kwani zinatakiwa kumnufaisha mkulima na Rais wetu Dkt Samia Suluhu ameweka nguvu kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri na bora”Alisema

Aidha alisema kwamba wale ambao wanafanya hivyo wanataka kufifisha juhudi za Serikali ambazo ni kuona wakulima wa zao hilo wananufaika nalo na hatimaye kuweza kujikwamua kiuchumi na kubadilisha maisha yao hivyo hawatakuwa tayari kuona zinakwamishwa kwa namna yoyote ile.

Kaimu Meneja huyo alisema mauzo ya korosho msimu uliopita yalikuwa ni tani 741 kwenye mnada uliofanyika wilayani Mkinga na kufanikisha kuingiza fedha kiasi cha Sh.Milioni 703 ambazo wakulima wa zao hilo wameweza kunufaika nalo.

Akizungumzia suala la udhibiti ubora wa zao hilo alisema kwamba wa sasa wamekuwa wakitoa mafunzo kwa wakulima ili kuweza kulima kilimo chenye tija ili kudhibiti ubora kuhakikisha unakuwa mzuri kabla ya kwenda sokoni ambapo wamekuwa wakiuza kwenye mfumo rasmi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.