ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 28, 2023

RAIS SAMIA ATEUA BOSI MPYA USALAMA WA TAIFA.

 


Rais Samia Suluhu Hassan akimuapisha Balozi Ali Idi Siwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa leo Agosti 28, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Massoro aliteuliwa kushika nafasi hiyo Januari 3 mwaka huu na kudumu kwenye ofisi hiyo nyeti kwa miezi nane kabla ya kuteuliwa kuwa balozi.

Kabla ya kupewa jukumu hilo Massoro alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu na Mkurugenzi wa Shughuli za Ndani wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa Balozi Siwa ameapishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam tayari kuitumikia nafasi hiyo nyeti na muhimu kwa Usalama wa Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Balozi Siwa alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko

wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) nafasi aliyohudumu tangu Septemba 20, 2018.

Kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda kwa takribani miaka mitatu kuanzia 2015 hadi 2018.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.