ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 12, 2022

MBUNGE DR KABATI NA MNEC MTEWELE WAUNGANA KUPINGA UKATILI KWA WAELEMAVU IRINGA.

 

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa viti kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa viti kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wakigawa vifaa kwa ajili ya walemavu mkoani Iringa 
 Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele na Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati wakizundua mchezo wa mpira wa kikapu wakati wa kongamano la watu walemavu mkoani Iringa

Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele na Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati wakizundua mchezo wa mpira wa kikapu wakati wa kongamano la watu walemavu mkoani Iringa


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati na mjumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi (CCM)  Theresia Mtewele wameungana kwa pamoja kupinga ukatili wa kijinsia hasa kwa watu wenye ulemavu mkoani Iringa na Tanzania kwa ujumla.

Akizungmza wakati wa Kongamano maalum lililolenga kupinga ukatili wa kijinsia pamoja na kutoa elimu ya Sensa ili kuwajengea uelewa na kujitokeza kuhesabiwa katika zoezi la Sensa linalotarajiwa kufanyika Mwezi nane Mwaka huu,MNEC Mtewele alisema kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia mkoa wa Iringa yamekuwa yakitokeza mara kwa mara hivyo ni lazima kuyakomesha matukioa hayo.

MNEC Mtewele alisema kuwa wananchi wa Iringa wanapaswa kutambua madhara yanayotokana na ukatili wa kijinsia kwa jamii husika kwa kuwa kumfanyia mtu ukatili ni jambo ambalo halikubariki katika jamii yoyote ile ya kitanzania.

Alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa Mkoa huo unaongoza kwa ukatili wa kijinsia na kwamba jamii yote hususani wakazi wa Mkoa huo wanapaswa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali katika kutokomeza vitendo hivyo kama anavyofanya Mbunge Kabati.

“Ni aibu sana na fedheha kwa mkoa wetu kuongoza katika vitendo vya ukatili wa kijinsia, tunapaswa kupiga vita kwa nguvu zetu zote na mtu akikutwa na hatia ya kuhusishwa na vitendo hivi anapaswa kuchukuliwa hatua kali hata kufungwa maisha” alisema MNEC Mtewele huku akionesha kukasirishwa na vitendo hivyo.

katika hatua nyingine amezungumzia umuhimu wa watu wenye ulemavu kushiriki katika Sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika mwezi wa nane mwaka huu na kuhimiza kuhesabiwa kwa watu wenye ulemavu na kwamba zoezi hilo  litaifanya Serikali kutambua idadi ya watu hao na hivyo kupata huduma kwa urahisi kutokana na mahitaji yao na maeneo walipo.

“Ndugu zangu naomba sana kuhamasisha wazazi na walezi kuhakikisha watu wote wenye ulemavu tulinao majumbani wanahesabiwa, usimfiche mtu mwenye ulemavu kwani kwa kufanya hivyo utaifanya Serikali kukosa idadi yao na hivyo kushindwa kuwafikia kuwapatia huduma zao wanazostahili” amesisitiza MNEC Mtewele

 

MNEC Mtewele alimazia kwa kumpongeza Mbunge Ritta Kabati kwa hatua yake ya kusaidia watu wenye mahitaji maalum na kwamba kwa kufanya hivyo anaunga mkono jitihada za Serkali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia na vitendo vya ukatili hasa kwa watoto na walemavu.


Awali akizungumza wakati wa kongamano hilo mbunge DR Ritta Kabati alisema kuwa  imekuwa ni ndoto na kiu yake ya muda mrefu pia imetokana na kushuhudia changamoto nyingi wanazokumbana nazo watu wa makundi maalum hususani wenye ulemavu, wazee, watoto, yatima na  wanawake ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri a Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan za kupinga ukatili wa Kijinsia.

 

Mgeni Rasmi kutokana na changamoto hizo nilianza
kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha napunguza au kuondoa changamoto hizo kabisa” alisema DR Kabati

Alisema kuwa amekuwa akiuliza mara kwa mara maswali na hoja zinazohusu watu wenye Ulemavu Bungeni ili kutafuta ufumbuzi ikiwemo mabadiliko ya kisheria na sera mbalimbali kuendana na mazingira yao.


Dr Kabati alisema kuwa aliamua kuanzisha kampeni maalum ya kusaidia vifaa saidizi ikiwemo fimbo, basikeli, mafuta na hata kuboresha miundombinu katika baadhi ya maeneo ili wasikutane na changamoto hiyo.

Aidha, ameongeza kuwa baada ya kuona hali ya uhitaji katika jamii ni kubwa, aliamua kuanzisha Taasisi maalum ya kushughulikia changamoto zinazowakabili  watu waliopo kwenye makundi maalum inayoitwa RITTA KABATI TRUST FUND, ambayo itajihusisha moja kwa moja kutafuta ufumbuzi wa changamoto za watu wenye mahitaji maalum kwa kuwafuata kwenye maeneo yao na kuwatambua ili kufanya uratibu wa kuwasaidia.

“Taasisi hii inalenga Kukuza utu na heshima kwa watu wenye ulemavu na kutoa ushauri wa matibabu bila malipo kwa walemavu pamoaja na kusaidia miradi na shughuli nyingine za kiuchumi zinazoendeshwa na watu wenye ulemavu” alisema DR Kabati.

Aidha amebainisha kuwa kazi nyingine ni kuanzisha na kudumisha vituo vya walemavu ili kusaidia
jamii na kujihusisha katika michezo hususani ya watu wenye ulemavu kwa k
uanzisha mashindano mbalimbali ya michezo na burudani katika Mkoa wa Iringa. 

Kazi nyingine ni pamoja na kusaidia programu na mipango inayolenga kuwaelimisha na kwafahamisha wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu kuhusu changamoto mahususi zinazowakabili watoto wenye ulemavu na jinsi ya kuwatunza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.