ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 12, 2025

WAZIRI KIKWETE AKOSHWA NA MAANDALIZI YA UWASHWAJI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA MKOA WA PWANI

 VICTOR MASANGU/KIBAHA/PWANI

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, vijana,ajira na watu wenye ulemavu  Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka vijana wa halaiki ambao  wamechaguliwa kushiriki  katika maandalizi ya uwashwaji wa  Mwenge  wa uhuru Kitaifa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kuwa wazalendo na nchi yao na kutunza na kuzilinda rasilimali za Taifa.

 Ridhiwani ameyasema hayo wakati alipofanya ziara kwa ajili ya kutembelea na kugagua  mwenendo na maandalizi katika eneo la uwanja  wa shirika la elimu Kibaha ambapo utakaotimika kwa ajili ya uwashwaji wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa ikiwa sambamba na kuzungumza na vijana hao na kuwahimiza kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha maandalizi.

Naye  Injinia  kutoka  ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Charles  Kabeho ambaye pia ni msimamizi wa ukarabati wa eneo la uwanja utakaotumika  kuwashiwa Mwenge wa uhuru amebainisha kwamba  kwa sasa ukarabati  kwa sasa umeshafikia  asilimia 75.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge amebainisha kwamba maandalizi yote kwa ajili ya kuelekea katika  tukio  la kuwasha Mwenge wa Uhuru Kitaifa yanaendelea vizuri katika maeneo ya miundombinu ya barabara, nishati ya umeme, maji na kwamba  hadi  sasa hali ya ulinzi na usalama imeimarishwa kwa kiwango kikubwa.

Sherehe za uwashwaji rasmi  wa  Mwenge wa uhuru kitaifa  zinatarajiwa kufanyika rasmi Aprili 2 mwaka huu katika viwanja vya shirika la  Elimu Kibaha vilivyopo Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani ambapo viongozi mbali mbali wa  ndani na nje ya nchi wanatarajia kushiriki katika tukio hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.