ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 11, 2019

CECAFA yYAWAJIBU SIMBA NA YANGA BAADA YA KUSUSIA KAGAME CUP.

Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesema mashindano ya Kagame Cup 2019 yataendelea licha ya kutokuwapo Simba na Yanga. Amesema Yanga ni timu isiyo na msaada, ndio sababu hufungwa 5-0 au 6-0 kwenye mashindano ya kimataifa. Mashindano hayo ya timu 16 yatafanyika Julai 17-21.

Utakumbuka hapo jana Klabu ya Yanga imesema haitoshiriki michuano ya Kagame Cup yatakayofanyika mwezi Julai 2019, jijini Kigali, Rwanda kwa sababu, wachezaji wengi wamemaliza mikataba, wengine wapo na timu ya taifa, na waliobaki wapo mapumziko.
Nicholas Musonye

Wakati hayo yakijiri, tayari Simba SC ilishatangaza kuwa haitoshiriki mashindano hayo, uamuzi huo umetokana na ratiba ya mashindano hayo kuingiliana na ratiba ya maandalizi ya msimu ujao wa Ligi ya Bingwa AFRIA (CAFCL) na Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) 2019/2020.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.