Wakati wa kuliombea taifa la Tanzania ilikuwa ni tofauti na tulivyozoea kwani watu waliimba wimbo huu kwa njia ya kuabudu na watu walibubujikwa hisia.
CHANZO: http://www.vipajihalisi.blogspot.com/
Mwandishi wa BBC Karen Allen akiwa Libya anasema jamii zinazopingana zimekua zikipigania eneo ambalo zamani lilidhibitiwa na wafuasi wa kanali Gaddafi.
Wapiganaji toka Zawia wakifurumisha roketi kuelekea eneo la makazi ya watu wa kabila la Warcafana umbali wa maili 25 toka mji wa Tripoli.
"Siyo shambani bali naelekea uwanja wa ndege"- Wazee wa safisha safisha.
Mvua kubwa iliyonyesha leo jijini Mwanza kwa takribani masaa manne imeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za usafiri na usafirishaji kwa njia ya anga.
Hali halisi....hatoki mtu...!!
kwasababu za kiusalama hakuna ndege iliyoruhusiwa kutoka au kuingia Air port Mwanza.
Hali ilikuwa mbaya zaidi majira ya saa mbili asubuhi ambapo maji mengi yaliyokuwa yakitiririka kutoka eneo la mwinuko kaskazini mwa kiwanja cha ndege Mwanza, yalisababisha taswira ya uwanja kubadilika na kuwa kama sehemu ya mto mkubwa unaotiririsha maji kuelekea ziwa victoria.
Pichani ni kama ndege iliyogota katikati ya shamba la mpunga kumbe laaa!! ni ndege iliyo katika eneo stahiki la maegesho ya ndege.
Wafanyakazi mbalimbali kiwanjani hapo wakishughulika kusafisha njia za ndege mara baada ya magugu na tope jingi kutanda eneo hilo.
Kikazi zaidi...kama shambani vile.
Hawa ndege sijui walitoka wapi!!! Naskia ni hatari sana kwa ndege ndogo za abiria.
Chekshia ngazi za ndege....
Wafanyakazi wa idara tofauti kiwanjani hapo wakihaha kuzima swichi za umeme kiwanjani hapo mara baada ya kina cha maji kuanza kupanda taratibu kikitishia usalama.
Wafanyakazi sekta ya mizigo walifanya kazi ya ziada kunusuru mizigo ilokuwa tayari imepakiwa kitengo cha mizigo isilowe.
Mara baada ya maji kupungua unaweza kuona jinsi miundo mbinu hasa njia za ndege ilivyoathirika.
Pata picha kama ndege zingeruhusiwa kuondoka au kutua wakati wa mafuriko ile hali tayari njia zandege zishaharibika......!!!!!???!!.
Hapa unaambiwa ni hali imetulia kwa Ofisi zetu kiwanjani.
Mbunge wa Monduli Edward Lowasa akipeana mkono na baadhi ya wanafunzi wa shule ya wasichana Loreto mara baada ya kupokea mchango wa shule hiyo kwa ujenzi wa wa Kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato jijini Mwanza.
Mazingira ya kanisa la nyakato.
Jumla ya shilingi milioni 200 zimepatikana leo na kuvuka lengo la shilingi milioni 150, katika harambee ya kusisimua ya Kumalizia Ujenzi wa Kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato jijini Mwanza harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Monduli Mh.Edward lowasa.
Waziri mstaafu ambaye ni mbunge wa Monduli Edward Lowasa akipokea Cheti cha kutambua mchango wake kusimamia vyema harambee za jamii na zawadi ya mbuzi toka kwa kamati ya ujenzi kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato Mwanza, mbuzi alinadiwa na kununuliwa na Papaa King kwa dola 100.
ONE LOVE Wenje $ Masha.
Akinamama walisimama kidete kuhakikisha lengo linafikiwa hapa Mama Kemilembe akiwasilisha mchango wake kwa mgeni rasmi.
"Kaka zimetimiaa" ni Mbunge wa Rolya Lameck Airo (shoto) na mfanyabiasha maarufu jijini Mwanza 'Six'.
Sehemu ya waumini waliofurika kwa wingi kufanikisha harambee hiyo.
Ni kanisa kubwa lililowekewa lengo na waumini wake kukamilika ujenzi na watu kusali ndani mwake katika ibada ya sikukuu ya Krismas ya mwaka huu 2011.
Marafiki wa mh. lowasa, Mkurugenzi wa Gold Crest Mr. Manga, Papaa King na Naftari Njoroge walijitutumua kweli kwenye harambee hiyo.
Mkazi wa jiji Mzee Ramadhani naye alialikwa kwenye harambee hiyo, hapa akimkabidhi Cash' shilingi laki 5 mchangishaji namba mbili mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Christopher Mwita Gachuma ambaye ni miongoni mwa waliojitokeza kwa dhati kufanikisha.
Lowasa alitumia ufundi mkubwa kuendesha harambee hiyo, pichani Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje akiwa kikaangoni na hatimaye aliwasilisha fungu lake na ahadi za marafiki zake walio mbali.
Wakurungenzi wa EF DOOR nao hawakuiangusha safu, walishiriki kikamilifu.
Mbunge wa Rolya, bw. Lameck Airo upande wake alichangia kiasi cha shilingi milioni 5.
Picha ya pamoja mgeni rasmi na Kwaya kuu ya kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato Mwanza.
Watu Mbali Mbali wakiwa wanakimbia ili kujiokoa na Hatari katika eneo hilo.
Wamachinga wakiwa Tayali kwa ajili ya Kupambana na FFU wakati wa tukio hilo
Baadhi ya wananchi wakiwa wameokoka katika eneo hilo
Polisi wakijalibu Kuzuia Ghasia katika eneo hilo na kufukuza Wamachinga.