ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, November 13, 2011

LOWASA AFANIKISHA KUVUKA LENGO UJENZI KANISA LA ROMAN CATHOLIC PAROKIA YA NYAKATO MWANZA, AHAMASISHA WAUMINI NA MARAFIKI ZAKE WACHANGA MILIONI 200

Jumla ya shilingi milioni 200 zimepatikana leo na kuvuka lengo la shilingi milioni 150, katika harambee ya kusisimua ya Kumalizia Ujenzi wa Kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato jijini Mwanza harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Monduli Mh.Edward lowasa.

Waziri mstaafu ambaye ni mbunge wa Monduli Edward Lowasa akipokea Cheti cha kutambua mchango wake kusimamia vyema harambee za jamii na zawadi ya mbuzi toka kwa kamati ya ujenzi kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato Mwanza, mbuzi alinadiwa na kununuliwa na Papaa King kwa dola 100.

ONE LOVE Wenje $ Masha.
Miongoni mwa viongozi walioitikia harambee hiyo ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Nyamagana Lawrence Masha (kulia) aliyechanga shilingi milioni 3.5, kisha milioni 1.5 toka kwa marafiki zake na laki moja aliyomwongezea mbunge Mama Hewa, ile hali Mbunge wa sasa Ezekiel Wenje (kushoto) kwa upande wake alichanga shilingi milioni 1.5.


Akinamama walisimama kidete kuhakikisha lengo linafikiwa hapa Mama Kemilembe akiwasilisha mchango wake kwa mgeni rasmi.

"Kaka zimetimiaa" ni Mbunge wa Rolya Lameck Airo (shoto) na mfanyabiasha maarufu jijini Mwanza 'Six'.

Sehemu ya waumini waliofurika kwa wingi kufanikisha harambee hiyo.

Ni kanisa kubwa lililowekewa lengo na waumini wake kukamilika ujenzi na watu kusali ndani mwake katika ibada ya sikukuu ya Krismas ya mwaka huu 2011.

Marafiki wa mh. lowasa, Mkurugenzi wa Gold Crest Mr. Manga, Papaa King na Naftari Njoroge walijitutumua kweli kwenye harambee hiyo.

Mkazi wa jiji Mzee Ramadhani naye alialikwa kwenye harambee hiyo, hapa akimkabidhi Cash' shilingi laki 5 mchangishaji namba mbili mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Christopher Mwita Gachuma ambaye ni miongoni mwa waliojitokeza kwa dhati kufanikisha.

Lowasa alitumia ufundi mkubwa kuendesha harambee hiyo, pichani Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje akiwa kikaangoni na hatimaye aliwasilisha fungu lake na ahadi za marafiki zake walio mbali.

Wakurungenzi wa EF DOOR nao hawakuiangusha safu, walishiriki kikamilifu.

Mbunge wa Rolya, bw. Lameck Airo upande wake alichangia kiasi cha shilingi milioni 5.

Picha ya pamoja mgeni rasmi na Kwaya kuu ya kanisa la Roman Catholic Parokia ya Nyakato Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.