ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 15, 2011

YEHOVA YU HAI LIVE TOUR ILIVYOFANA MWANZA

Mwimbaji mahiri wa kimataifa wa muziki wa injili John Lisu akimtambulisha Mke wake Nelly Lisu katika Tamasha lililopewa jina la JEHOVA Yu Hai Tour lililofanyika tarehe 6 November 2011, ambapo Lisu aliongozana na Timu ya Wapiga Vyombo na waimbaji kutoka jijini Dar.

Mimi hupenda kumwita Dogo lakini ni mmoja wa waimbaji anayekuja kwa kasi katika Tasnia ya muziki wa injili na pia mtangazaji wa Radio ya kikristo ya 91.9 ALIVE FM ya Jijini mwanza Adolph Robert Nzwalla akihusika kikamilifu kuhakikisha jina la Yesu linainuliwa.

Wakati wa kuliombea taifa la Tanzania ilikuwa ni tofauti na tulivyozoea kwani watu waliimba wimbo huu kwa njia ya kuabudu na watu walibubujikwa hisia.

Mrs Matata na mwanae Kivila Matata nao waliguswa na roho kuhudhuria tamasha hili la aina yake lililofanyika kwa mara ya kwanza jijini hapa.

Bishop Murisa Akifanya maombezi.

Full upako

Watu wakimwadhimisha Mungu.
CHANZO: http://www.vipajihalisi.blogspot.com/

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.