🚨𝗠𝗸𝘂𝘆𝘂𝗻𝗶: 𝗠𝗮𝗮𝗳𝗮 𝘆𝗮 𝗺𝘃𝘂𝗮 𝘆𝗮𝗺𝗳𝘂𝗻𝗴𝗮 𝗺𝘁𝗮𝗮, 𝘄𝗮𝗳𝗮𝗻𝘆𝗮𝗯𝗶𝗮𝘀𝗵𝗮𝗿𝗮 𝘄𝗮𝗸𝗮𝘁𝗮 '𝗛𝗮𝘁𝘂𝗺𝘄𝗶 𝗺𝘁𝗼𝘁𝗼 𝗱𝘂𝗸𝗮𝗻𝗶'
.Majira ya asubuhi ya leo tarehe 10/03/2026 eneo la Mkuyuni lilishuhudia mafuriko makubwa baada ya mvua kuendelea kunyesha, hali iliyofanya barabara zisipitike na maji kujaa kwa kiwango kinachoharibu biashara na maduka kandokando ya barabara.
.
Mvua ilianza mdogomdogo mapema alfajiri na kuongezeka kuanzia saa 2:30 hadi 4:00 asubuhi, ikichapa ile yenyewe, ikisababisha wateja kukosa uwezo wa kufika sokoni na wafanyabiashara kulazimika kufunga maduka.
.
“Maji yalikuja ghafla na kujaa dukani nikalazimika kupandisha juu bidhaa zote nilizokuwa nimeziweka chini sakafuni — hatumwi mtoto dukani,” alisema mfanyabiashara mmoja wa sokoni, akieleza wasiwasi wa wafanyabiashara waliokuwa wameweka bidhaa mafuta za mauzo.
.
Hadi sasa mamlaka za mkoa au wilaya hazijatoa taarifa rasmi kuhusu uzito wa uharibifu au idadi ya wahasiriwa.
.
#jembehabari
#DriveMix
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment