ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 17, 2024

WASHUKIWA WAWILI ZAIDI WAKAMATWA HUKU MSHUKIWA MKUU AKIZUILIWA KWA SIKU 30

Collins Khalusha alizuiliwa kwa siku 30 kutokana na mauaji ya Kware. 

Nairobi - Maafisa wa upelelezi kutoka Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) wamewatia mbaroni washukiwa wawili zaidi wanaohusishwa na mauaji ya kinyama katika eneo la Kware, mtaa wa mabanda wa Mukuru kwa Njenga jijini Nairobi. 

Kwa nini Amos Momanyi Mogusu alikamatwa? Mnamo Jumapili, Julai 14, miili kadhaa iliyokatwakatwa ilipatikana katika eneo la kutupa taka na umma. Katika taarifa, DCI ilifichua kukamatwa kwa Amos Momanyi Mogusu, ambaye alinaswa katika eneo la City Cabanas. 

Kulingana na maafisa hao wa upelelezi, Momanyi alipatikana akiwa na simu ya mmoja wa waathiriwa, Roselyn Akoth Ogongo, ambaye mabaki yake yalitambuliwa na jamaa zake katika Makafani ya Nairobi. 

Ni vitu gani vya waathiriwa wa mauaji ya Kware vilipatikana? Baada ya kuhojiwa, Momanyi aliongoza maafisa wa upelelezi kwa mshukiwa wa tatu aliyejulikana kwa jina la Moses Ogembo ambaye anasemekana alimuuzia simu hiyo ya rununu. 

Katika nyumba ya Ogembo, wapelelezi walipata simu 154 za mitumba, na alikiri kuwa alinunua simu zilizotumika kutoka kwa mshukiwa mkuu, Collins Khalusha. "Baada ya kukamatwa kwa Amos Momanyl Mogusu katika mtaa wa Cabanas na kupatikana kwa simu ya rununu jana, aliongoza wapelelezi hadi kwa nyumba ya Ogembo iliyoko Mukuru kwa Reuben, ambaye alipatikana na jumla ya simu 154 zilizotumika zimefichwa nyumbani kwake," DCI ilisema. 

Wakati huo huo, makachero hao walipewa siku 30 kuendelea kumzuilia Khalusha ili kukamilisha uchunguzi wa madai ya mauaji hayo. 

Je, Collins Khalusha alilazimishwa kukiri makosa ya mauaji ya Kware? Huku hayo yakijiri, Khalusha, mshukiwa wa mauaji ya takriban wanawake 42 na kuwatupa kwenye machimbo eneo la Kware, aliwashutumu polisi kwa ukatili. 

Kupitia kwa wakili wake, John Maina Ndegwa, Khalusha alidai aliteswa hadi kukiri mauaji hayo. Akiwa amefikishwa mbele ya Hakimu Mkuu Irene Gichobi katika Mahakama ya Makadara, Ndegwa aliomba mahakama imruhusu kutafuta matibabu, akiongeza kuwa madai dhidi yake ni ya kuchekesha. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.