ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 17, 2024

WILLIAM RUTO KUBUNI OFISI YA JENERALI MKUU WA KUCHUNGUZA VIFO.


Nairobi - Wizara ya Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa imefichua mipango ya kubuniwa kwa Ofisi ya Mkuu wa Uchunguzi wa Vifo. 

Katika taarifa siku ya Jumanne, Julai 16, wizara hiyo ilieleza kuwa ofisi hiyo itabuniwa chini ya Sheria ya Kitaifa ya Huduma ya Wachunguzi wa Vifo 2017. 

Wizara hiyo ilifichua kuwa ilimshauri Rais William Ruto kuunda afisi ambayo itachunguza mauaji yanayohusishwa na ukatili wa polisi. 

Kulingana na wizara hiyo, afisi hiyo itahakikisha uwajibikaji na uwazi katika visa vya vifo vinavyoshukiwa. 

 “Wizara imependekeza kwa Mheshimiwa Rais aanzishe mchakato wa uanzishaji wa Ofisi ya Mchunguzi Mkuu wa Vifo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma ya Wachunguzi wa Kitaifa ya mwaka 2017 ili kuchunguza vifo vikiwemo vilivyotokana na polisi, Ofisi ya Mchunguzi Mkuu pia itahakikisha uwajibikaji na uwazi katika visa vya vifo vinavyoshukiwa," ilisoma taarifa hiyo kwa sehemu.

Ni onyo gani ilitolewa kwa polisi? Wizara hiyo pia iliwataka polisi kujizuia wanapokabiliana na waandamanaji kote nchini, ikisisitiza kujitolea kwake kuheshimu utakatifu wa maisha ya binadamu. 

Hata hivyo, polisi wamepewa mwanga wa kijani wa kutumia nguvu zinazofaa wakati vitendo vya uhalifu vinaposhinda maandamano ya amani. 

 “Polisi wanaweza kulazimika kutumia nguvu ya kuridhisha pale wanapojitenga na matukio mahususi ya maandamano yanapofikia vitendo vya uhalifu, vikiwemo fujo, uporaji, uchomaji wa mali, uvunjifu wa magari,” ilisema wizara hiyo. 

Maafisa wa polisi pia wamepewa notisi kwamba kukamatwa kunategemea Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, ambayo inaeleza jinsi ukamataji hutekelezwa na kuwekwa kizuizini na kufikishwa mahakamani kwa washukiwa. 

Serikali ilitoa wito kwa wafanyabiashara na wamiliki wa majengo binafsi wanaolinda mali zao kuwasiliana na mamlaka ili kusimamia usalama kwa utaratibu 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.