ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 9, 2024

WATANZANIA WATAKIWA KUIENZI NA KUITUNZA AMANI ILIYOPO NCHINI

 

 


Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo akizungumza wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga




Na Oscar Assenga,KOROGWE.

WATANZANIA wametakiwa kuienzi amani iliyopo hapa nchini ambayo ni tunu kubwa iliyoacha na waasisi wa Taifa hili na wasikubali kamwe ichezewe kutokana na kwamba kufanya hivyo itaondoa umoja wetu ambao ni chachu ya maendeleo.

Wito huo ulitolewa na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Korogwe Julius Mbwambo wakati wa halfa ya Futari iliyoandaliwa na Kanisa hilo kwa makundi maalumu yaliyopo kwenye hali ya chini na kufanyika katika Stendi ya Kijazi wilayani Korogwe mkoani Tanga

Alisema wao kama Kanisa wanatambua kwamba amani ni kitu muhimu sana kwa ustawi wa jambo lolote lile hivyo ni lazima itunze na iendelee kuenziwa na ndio maana wameona mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufuturisha kutokana na umoja uliopo na kwamba wao ni ndugu moja.

Futari hiyo iliandaliwa na Kanisa hilo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali ambapo ililenga makundi ya Makondakta,Waendesha bajaji,Wajasiriamali ,Wamachinga ambapo pia viongozi wengine wa kiserikali nao walishiriki lengo likiwa ni kuhimiza umoja na kudhimisha amani.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa futari hiyo Mchungaji wa Kanisa hilo Mbwambo alisema kwamba wao kama viongozi wa dini ni kuonyesha umma kwamba katika suala la mungu ni lazima kuwe na umoja na mshikamano kutokana na kwamba wao ni wametoka kwa baba mmoja.

“Futari hii ni kuonyesha umoja sisi kama kanisa na tunaendelea kusisitiza mshikamano na amani kwa sababu hivyo ndio vitu muhimu kwa ustawi wa jamii yoyote ile hivyo tuendelee kuitunza na kuienzi na tusiwafumbie macho wale ambao watakaojaribu kuichezea”Alisema

Hata hivyo alitoa wito kwa taasisi na watu wenye uwezo kuona namna ya kuwasaidia wahitaji wanapokuwa kwenye mwezi mtufuku wa ramadhani kuhakikisha wanayagusa makundi yaliyokuwa kwenye hali ya chini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.