ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 8, 2024

RWANDA YAADHIMISHA MIAKA 30 YA MAUAJI YA KIMBARI

 


TAIFA la Rwanda limeadhimisha miaka 30 tangu yafanyike mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ya Watutsi na Wahutu, ambayo yalichukua uhai wa watu takribani 800,000 ikiwa ni tukio baya zaidi la mauaji ya karne ya 20 yaliyowahi kushuhudiwa katika bara la Afrika.


Wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika jana Rais wa Rwanda Paul Kagame, aliwasha mwenge ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji hayo kwenye eneo la kumbukumbu ya mauaji ya kimbari katika mji wa Kigali.

Mauaji hayo yalitokea Aprili 7 mwaka 1994 na kwamba zaidi ya wahanga 250,000 wanaaminika walizikwa katika eneo hilo la kumbukumbu.


Bendi ya jeshi ilipiga nyimbo za huzuni, wakati Rais Kagame alipoweka mashada ya maua kwenye makaburi ya halaiki, akiwa amezungukwa na viongozi wa kigeni wakiwemo wakuu kadhaa wa nchi za Afrika na aliyekuwa Rais wa Marekani wakati wa mauaji hayo Bill Clinton.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.