ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 8, 2024

MKUU WA MKOA WA LINDI ASISITIZA UBORA WA MIRADI KUELEKEA MBIO ZA MWENGE.

 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka wakurugenzi na waratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kuzingatia ubora wa miradi itakayopitiwa katika Halmashauri za Mkoa wa Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka wakurugenzi na waratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kuzingatia ubora wa miradi itakayopitiwa katika Halmashauri za Mkoa wa Lindi.
Na Fredy Mgunda, Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka wakurugenzi na waratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kuzingatia ubora wa miradi itakayopitiwa katika Halmashauri za Mkoa wa Lindi.


Mhe. Telack ameyasema hayo jana jumamosi tarehe 06 Mei 2024 kwenye kikao cha pili cha maandalizi ya mbio za Mwenge zinazotarajiwa kukimbizwa Mkoa wa Lindi mwezi Mei mwaka huu 2024.


Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Telack amesema kuwa miradi yote itakayochaguliwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru ni lazima iwe na ubora wa viwango vya kuridhisha ikiwemo uhalisia wa fedha iliyotumika.


Ameongeza kuwa pamoja na kuzingatia ubora wa miradi hiyo lakini pia uwepo Wahandisi ujenzi waliosimamia miradi hiyo ni muhimu hasa kwenye ufafanuzi wa taarifa za mradi husika kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.


Mhe. Telack amewasisitiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha uandaaji wa miradi hiyo unazingatia maelekezo yote ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 ikiwemo ujumbe wake unaolenga utunzaji wa Mazingira.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.