ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 9, 2024

KINANA, RC KUNENGE WAFIKA RUFIJI KUWAFARIJI WANANCHI WALIOPATWA NA MAFURIKO


VICTOR MASANGU,
RUFIJI

Wananchi wa wilaya ya Rufiji kata  chumbi A na kata ya Muhoro Mkoa wa Pwani  wamehakikishiwa kupatiwa misaada ya haraka kulingana na mahitaji ambayo wanatakiwa kupatiwa kwa kipindi hiki ambacho wameathirika kutokana na janga la mafuriko. 


Kinana ameyasema hayo leo 9 , 04 ,2024 Mhe . Abdulirahmani Kinana wakati alipoenda kutoa pole kwa waathirika hao pamoja na kutoa salamu za Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani kwa wananchi wote ambapo ameahidi kuwa ataagiza kila kinachowezekana kifanyike ili wananchi wasiendelee kuathirika .


Pia Mhe . kinana amesema kuwa nae Waziri mkuu Kassim Majaliwa tayali anashughulikia swala hilo ambapo mpaka kufikia kesho baadhi  ya vifaa vitakua vimeshafika lakini kwasasa miongoni mwa vifaa vilivyopo ni pamoja na blanketi , magodoro , mahema na vyakula ila havitoshelezi kwa wahanga hao .


 Aidha  Makamu mwenyekiti Kinana ametumia nafasi hiyo kuwapongeza viongozi wawili ambao ni mbunge wa jimbo la ikwiriri pamoja na mbunge wa jimbo la kibiti kwakua na ushirikiano kwa wananchi wake wanaowaongoza . 


 Nae Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe . Abubakar Kunenge amesema kuwa Maeneo ambayo yaliopatwa na  athari ni jumla ya ekali elfu 34 ,na  wananchi waliopata athari ni takribani kaya elfu 33 na jumla ya idadi yao ni elfu 88 lakini pia katika wilaya hiyo ya chumbi vifo vilivyopatikana ni wiwili ambavyo ni mama pamoja na mtoto .


Sambamba na hilo Mhe. kunenge ameomba kuwa miongoni mwa misaada ambayo itatolewa kwa wahanga  iweze kuwafikia kwa wakati  walengwa wote wenye uhitaji wa misaada hiyo .








Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.