ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 27, 2023

WANAUME WANNE WAMPIGA NA KUMUUA DADA YAO KISA SHAMBA LA URITHI.


Polisi nchini Uganda wanachunguza kisa ambapo wanaume wanne wanadaiwa kumuua dada yao kwa kumpiga katika Wilaya ya Rukiga, Kusini Magharibi mwa nchi hiyo.

Christine Kiconco mwenye umri wa miaka 41 anaripotiwa kuuawa na kaka zake - Innocent Tumwekwase, Samuel Atuhirwe, Christopher Bikorwomuhangi na Justus Mayumba - kufuatia mzozo wa ardhi.

Msemaji wa polisi wa eneo la Kigezi Elly Maate anasema kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa familia hiyo ilikuwa na mzozo mrefu kuhusu shamba walilorithi kutoka kwa mababu.

Kwa mujibu wa polisi, kaka hao wanne walipewa vipande vyao vya ardhi lakini wakavipiga mnada punde tu vilipofika katika umiliki wao.

Polisi wanasema kuwa wanne hao walianza kuwaandama dada zao wakitaka ardhi waliyopewa wasichana wa familia hiyo na sasa hilo limeishia katika mauti.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.