ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 27, 2023

WAZIRI MKUU WA TANZANIA AVUTIWA NA KASI UJENZI WA SGR MWANZA-ISAKA

 


Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa mwishoni mwa juma tarehe 26 Machi 2023 amekagua Mradi wa Ujenzi wa reli ya kisasa SGR Mwanza-Isaka, Kipande cha Tano cha Ujenzi wa reli awamu ya kwanza Dar es Salaam Mwanza.


Kipande hiki cha Mwanza-Isaka kina jumla ya kilometa 341, hadi kukamilika kwake kitagharimu shilingi Trilioni 3.062.



Kipande hicho kitakuwa na jumla ya vituo vya abiria 10 na vituo viwili vya mizigo vya Fela na Isaka.



Maendeleo ya ujenzi huo umefikia asilimia 28.03 na ujenzi wa tuta ni asilimia 58.4 sawa na kilometa 136 kati ya kilometa 249 za njia kuu.


Mradi huo umetoa ajira zaidi ya 6,720 na kandarasi ndogo zenye thamani ya shilingi bilioni 80 hadi sasa.


Baada ya kukagua mradi huo Mheshimiwa Majaliwa amesema amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo huku akitoa wito kwa wananchi wa maeneo hayo kuwa walinzi wa vifaa na mitambo inayotumika katika ujenzi huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.