ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 20, 2023

PASTA AMBAYE MWILI WAKE ULIHIFADHIWA KWA SIKU 579 AKITARAJIWA KUFUFUKA HATIMAYE AZIKWA.


Mhubiri ambaye alifariki mwaka 2021 jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini na mwili wake kuhifadhiwa na kuombewa akitarajiwa kufufuka hatimaye amezikwa.

Mwili wa pasta wa Gauteng - Siva Moodley - umekuwa katika makafani ya Johannesburg tangu Agosti 15, 2021 alipokumbana na mauti.Mwanzilishi huyo wa kanisa la The Miracle Centre lililo kaskazini mwa Johannesburg aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 53 baada ya kuwa mgonjwa.

Kwa mujibu wa ripoti ya awali ya jarida la OIL, familia ya Mooley na washirika wake wamekuwa wakizuru makafani hayo kusali ili afufuke.

Licha ya haya, meneja wa makafani hayo Martin du Toit aliwasilisha ombi katika mahakama ya Johannesburg akitaka ruhusa ili auzike au kuuchoma mwili wa Moodley.

Tangu kufa kwake, inaarifiwa ibada zimekuwa zikiendelea katika kanisa lake, zikiendeshwa na mke wake Jessie, na wanawe wawili David na Kathryn Jade.

 Ibada hizi hupeperushwa moja kwa moja kwenye mitandao ya kijamii. Hata hivyo inaarifiwa kuwa kanisa halijakiri kufariki kwa mhubiri huyo.

Kutokana na hilo, inadaiwa halijatangaza kifo chake kwenye mitandao ya kijamii wala kuwaambia washirika aliko pasta wao.

Pia imearifiwa kuwa akaunti za Moodley kwenye mitandao ya kijamii - hususan Facebook na Twitter - bado zinafaya kazi na jumbe kuanikwa hapo kila siku kanakwamba zinatoka kwake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.