ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 23, 2023

POLISI WAUWA MAJAMBAZI WAWILI, WAKUTWA NA MABOMU.

 


WATU wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wenye umri kati ya miaka 25 hadi 30 wameuawa na Jeshi la Polisi mkoani Kagera na kisha kukutwa na bunduki moja aina ya AK 47, risasi 25 na mabomu mawili ya kurusha kwa mkono.


Watu hao bado hawajafahamika, waliuawa Januari 21, 2023 na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Nyamiyaga wilayani Ngara kwa ajili ya kutambuliwa na kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kagera, William Mwampaghale amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Januari 21, 2023 saa 3:35 usiku katika maeneo ya Barabara ya Kumunazi kwenda Relenge, Wilaya ya Ngara.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.