ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 23, 2023

POLISI WAFUKUA KABURI LA KIJANA ALIYEONEKANA MTAANI.


JESHI la Polisi kwa kushirikiana na wananchi na wataalamu wa afya, wamefukua kaburi la kijana Henry James (28), aliyedaiwa kufariki Aprili 20, 2022 na kupatikana akiwa hai Desemba 22,2022.


Tukio hilo la ufukuaji wa kaburi umefanyika katika Kijiji cha Kandaga, wilayani Uvinza mkoani Kigoma leo Januari 22, 2023 na kukutwa mwili huo ambapo wamechukua sampuli na kupelekwa kwa mkemia mkuu wa serikali kwa ajili ya uchunguzi wa vina saba.

Lengo la ufukuaji huo wa kaburi linalodaiwa la kijana Henry ni kupata sampuli za vinasaba vya mwili huo na kulinganisha na sampuni za kijana huyo huyo anayedaiwa kuonekana uraiani akiwa hai mwishoni mwa mwaka jana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.