ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 23, 2023

'RUKSA YA RAIS MIKUTANO YA HADHARA KWA VYAMA VYA SIASA IMEKUJA MUDA MUAFAKA INGECHELEWA INGETUKOSTI'

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Mshauri wa Kamati ya Amani Mkoa wa Mwanza Mchungaji Dkt. Jacob Mutash wa Kanisa la EAGT Kiloleli anasema kuendelea kuwa na zuio hilo baadaye ingetugharimu, kwani yangetokea mambo makubwa ya hovyo ambayo huenda yangeichafua nchi na sifa zake kutambulika kama kimbilio la amani. "Sito shangaa kuona viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa wakimpongeza Mhe. Rais Dkt Samia kwa kuwa hili lina busara yenye heri kwa taifa" "Kinachotakiwa hapo ni kupokea heshima hiyo aliyotupa Mhe. rais kwa moyo wa shukurani na kumuenzi kwa kufanya siasa za amani kwani kama angenyamaza nani angefanya chochote?" amehoji Mchungaji Mutash na kisha akaongeza. "Hatuzuii wasibishane, Hatuzuii wasipingane bali wapingane kwa hoja na wapingane wasibigane" #MikutanoYaHadhara #Siasa #tanzania

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.