ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 27, 2022

TAZAMA WANAODAIWA KUMZIKA MTOTO AKIWA HAI WALIVYOPANDISHWA KIZIMBANI.

 MWANZA. Watu watatu akiwemo Mkazi wa kijiji cha Mahaha wilayani Magu mkoani Mwanza, Zawadi Msagaja (20) wamepandishwa kizimbani kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa kike mwenye umri wa miezi sita kwa kumzika shambani akiwa hai ili wapate mali.

Wengine katika kesi hiyo ya mauaji namba 7/2022 ambao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza na kusomewa shtaka la mauaji ya mtoto huyo ni dada yake Zawadi, Elizabeth Kaswa na mmewe, Mussa Mazuri ambaye ni mganga wa kienyeji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.