ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 13, 2022

WAFUASI WA RUTO WAPATA AJALI WAKIELEKEA UWANJANI KUSHUHUDIA UAPISHO.

 

Wafuasi wa Rais Mteule William Ruto kutoka kijijini Sugoi wamepata mkosi walipokuwa wakielekea Kasarani kushuhudia mtoto wao akiapishwa.

Tukio Hilo lilitokea mapema leo kabla ya uapisho baada ya basi la shule walilokuwa wakitumia kuhusika katika jali eneo la Sachagwan barabara ya Eldoret- Nakuru. 

Taarifa zinaarifu kuwa abiria 31 walipata majeraha mabaya wakati wa kisa hicho. 

Na kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema kuwa basi hilo lilipoteza mwelekeo na ndipo likaingia kwenye mtaro na kubingirika mara kadhaa. 

Waliojeruhiwa walikimbizwa hospitali ya kaunti ya Molo kwa matibabu huku safari yao ya kushuhudia Ruto akiapishwa ikaishia hapo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.