ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 30, 2022

MAHAKAMA YAKATAA KUMWACHILIA MSICHANA ALIYEUA JAMAA ZAKE WANNE HUKU MIILI IKIPANGIWA KUFUKULIWA

 


Mahakama imeamuru kuendelea kuzuiliwa kwa msichana wa miaka 15 ambaye alikamatwa kwa mauaji ya ndugu zake watatu na binamu yake. 

Mahakama imeagiza msichana huyo aendelee kuzuiliwa ili polisi wakamilishe uchunguzi wao. 

Hakimu Mkuu Mkaazi wa Mahakama ya Kikuyu Catherine amekubali ombi la polisi la kumzuilia mshukiwa kwa siku 14 zaidi ili kukamilisha uchunguzi. 

Polisi pia wanapanga kumfanyia uchunguzi wa kiakili msichana huyo ambaye alikiri kutekeleza mauaji hayo. 

Gavana Mwangaza Afichua Alirushiwa Usoni Mayai Yaliyooza Mshukiwa ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza atasalia rumande hadi Septemba 12 kesi hiyo itakapotajwa. 

Mshukiwa atekeleza mauaji ya jamaa zake wanne Msicha huyo kutoka Kaunti ya Kiambu alikiri kutekeleza mauaji hayo katika muda wa mwaka mmoja uliopita. 

Mshukiwa pia alikiri kuwa mwezi jana aliua binamu yake, mtoto wa umri wa miezi 20 kwa kumrusha katika kisimani nyumbani kwao katika kijiji cha Gathiga, kaunti ndogo ya Kabete.

 “Pia alikiri kumuua binamu yake a miezi 20 kwa kumrusha katika kisima nyumbani kwao mwzi jana. 

Leo babake alielekea katika kituo cha polisi cha Kikuyu na kuandikisha taarifa dhidi ya msichana huyo akimtuhumu kuua wanawe watatu,” taarifa ya DCI ilisema..

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.