ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 1, 2022

ROYAL TOUR NI PONGEZI KILA KONA

 


RAIS ya Jumuiya wa Wanafunzi wa Elimu ya Juu(TAHLISO), Frank Nkinda amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha uzinduzi wa filamu ya Royal Tour na kusisitiza kuwa Watanzania wote wapo nyuma ya jitihada anazozifanya kuitangaza Tanzania kimataifa.


Akizungumza ikiwa ni siku mbili tangu kuzinduliwa filamu hiyo uliofanyika jijini Arusha, Nkinda amesema kufanikisha hatua hiyo, Rais Samia anazidi kuonesha kwa vitendo dhamira yake ya kuiletea maendeleo Tanzania kupitia sekta ya utalii.


Amesema kuzinduliwa filamu hiyo inayoonesha vivutio mbalimbali vya utalii na kiutamaduni, kutazidi kuongeza idadi kubwa ya watalii wanaoingia nchini kwa lengo la kuja kuvitazama, hatua ambayo itasaidia kukuza pato la Taifa kutokana na fedha za kigeni.


Amewataka Watanzania wote kwa umoja wao kuendelea kumuunga mkono Rais Samia, ili aweze kutimiza malengo yake ya kuiletea nchi maendeleo, jambo ambalo pia litawezesha kuongezeka kwa kipato cha mtu mmoja mmoja.


Awali kabla ya kuzinduliwa kwa filamu hiyo Arusha juzi, Rais Samia alikuwa nchini Marekani aliposhiriki uzinduzi wa filamu hiyo ya Royal Tour katika Majiji mawili ya New York na Los Angeles.


Mtu mwingine mashuhuri aliyehudhuria ukiondoa mabilionea na wamiliki wa makampuni makubwa duniani ikiwemo watangazaji


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa filamu hiyo juzi, Rais Samia alisema matarajio mara baada ya kuzinduliwa, idadi ya watalii nchini itaongezeka mara mbili zaidi ya ilivyo sasa na kuliongezea Taifa mapato yatokanayo na sekta ya utalii.


Baada ya uzinduzi huo mkoani Arusha ulioudhuriwa na watu takribani 5000, Mei 7  filamu hiyo ya Royal Tour   itazinduliwa Zanzibar na Mei 8 uzinduzi rasmi utafanyika Dar es Salaam katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.