ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 1, 2022

KIONGOZI WA KIJESHI WA GUINEA ATANGAZA KIPINDI CHA MPITO CHA MIEZI 39

 


Mkuu wa utawala wa kijeshi nchini Guinea, Kanali Mamady Doumbouya, ametangaza kipindi cha miezi 39 ya utawala wa mpito kabla ya taifa hilo la magharibi mwa Afrika kurejea kwenye utawala wa kiraia.


 Akihutubia taifa usiku wa kuamkia leo, Kanali Doumbouya amesema baraza la taifa la kipindi cha mpito litawasilisha mapendekezo yake bungeni. Tangazo hili limekuja baada ya kuundwa kile kiitwacho "mfumo shirikishi wa mashauriano" mnamo mwezi Aprili. 


Hata hivyo, mkutano uliopitisha chombo hicho ulisusiwa na makundi kadhaa mashuhuri ya upinzani. Siku ya Ijumaa, serikali ya kijeshi ilikuwa imetangaza kuwa mkutano huo ulipendekeza kipindi cha mpito kiwe baina ya miezi 18 na 52. 


Lakini kwenye hotuba yake ya usiku wa jana, Kanali Doumbouya alisema ameamuwa kuchukuwa njia ya kati kati. Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) iliiweka Jumatatu iliyopita kuwa muda wa mwisho kwa utawala wa kijeshi wa Guinea kutoa ratiba inayokubalika ya kurejesha utawala wa kiraia, ama ukabiliane na vikwazo cha kiuchumi na kifedha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.