ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 7, 2022

AUAWA BAADA YA KUUZA GARI MNADANI.

 


Mfanyabishara na mkazi wa mtaa wa Kipondoda Wilaya ya Manyoni mkoani Singida, Sita John (45) amefariki dunia na mkewe kujeruhiwa baada ya kupigwa na kitu chenye ncha kali na watu wasiojulikana.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Machi 7, 2022 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Stella Mutabihirwa amesema kuwa tukio hilo limetokea Jumamosi Machi 05, 2022 wilayani Manyoni.


Kamanda huyo amesema siku ya tukio mfanyabiashara huyo alienda mnadani kuuza gari yake Sh15 milioni.


“Lakini badala ya kupewa fedha, alipewa ng’ombe (idadi haijajulikana) na fedha kiasi. Watu hawa wanaotaka kujipatia fedha kwa njia ya mkato, hawakujua kwamba mfanyabiashara Sita alipewa ng’ombe na fedha kiasi,”amesema.


Kamanda Stella amesema kuwa mkewe alijeruhiwa na kitu chenye ncha kali wakati akijihami kwenye tukio hilo.


Kamanda Stella amesema baada aya kupata taarifa ya tukio hilo, Polisi ilifanya msako na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye familia ya marehemu ilimtambua.


Amesema watu hao walifanikiwa kupora fedha ambayo kiasi chake bado hakijafahamika.


“Upelelezi juu ya tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na mahojiano na mtuhumiwa aliyekamatwa ili kuwafahamu watu anaoshirikiana nao katika matukio ya wizina mauaji” amesema.


 “Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Singida kuachana na vitendo vya kujitafutia mali kwa njia zisizo halali,”amesema kamanda huyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.