ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 7, 2022

UFILIPINO YAONGEZA UMRI WA KUANZA KUJAMIIANA KUTOKA 12-16

 


Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte amesaini sheria inayoongeza umri ambao mtu anaruhusiwa kufanya mapenzi kutoka miaka 12 hadi 16, katika juhudi za kuwalinda watoto dhidi ya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia. 


Chini ya Sheria ya Ulinzi Maalum wa Watoto dhidi ya Unyanyasaji, Unyonyaji na Ubaguzi, watu wazima ambao wana uhusiano wa kimapenzi na mtu mwenye chini ya miaka 16, kisheria wana hatia ya moja kwa moja ya ubakaji. 


Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto, UNICEF, kabla ya sheria hiyo, Ufilipino ilikuwa na kiwango cha chini zaidi duniani kwenye umri ambao mtu anapaswa kujamiiana, ikiwa nyuma ya Nigeria ambao kisheria ni miaka 11.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.