ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 8, 2022

MWANZA WAADHIMISHA KWA KISHINDO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.

 

Matukio mbalimbali katika picha: Maandamano ya wadau mbalimbali kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2022 ngazi ya Mkoa Mwanza yaliyoadhimishwa kwa kishindo katika uwanja wa Nyamagana, Machi 08, 2022 

Shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana KIVULINI ni miongoni mwa wadau muhimu walioungana na wanawake mkoani Mwanza kusherehekea Maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel aliyewakilishwa na Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Ngusa Samike.
Maandamano ya wadau wakiingia katika uwanja wa Nyamagana.

Siku ya wanawake ilikuja kutokana na vuguvugu la wafanyakazi mnamo mwaka 1908, na ikatambuliwa rasmi kama hafla ya kila mwaka na miongo kadhaa baadaye, mnamo 1975.

Mnamo mwaka 1908, zaidi ya wanawake 15,000 waliandamana katika jiji la New York kudai muda mfupi wa kufanya kazi, malipo bora na haki ya kupiga kura.

Chama cha Kisoshalisti cha Marekani kilitangaza Siku ya Kitaifa ya Wanawake ya kwanza nchini Marekani mwaka mmoja baadaye.

Mjerumani Marxist na mwanaharakati Clara Zetkin alikuwa mmoja wa waasisi wa utambuzi wa toleo la kimataifa la Siku ya Kitaifa ya Wanawake ya Marekani.


Mkurugenzi Mtendaji Shirika la KIVULINI, Yassin Ally akiongoza hamasa kwenye maandamano hayo.
Viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Amina Makilagi (katikati) wakiwa kwenye maadhimisho hayo.

Kila mwaka Machi 08, Umoja wa Mataifa husheherekea haki zilizopatikana kwa bidii za wanawake- na kuangazia changamoto ambazo bado ziko mbele katika kukomesha ubaguzi wa kijinsia katika karibu nyanja zote za maisha.

"Usawa wa kijinsia wa leo, kesho na endelevu" ndio kauli mbiu ambayo Umoja wa Mataifa umeichagua mwaka huu kuadhimisha kile kinachojulikana rasmi kama Siku ya Kimataifa ya Wanawake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.