ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 3, 2021

RONALDO HAKAMATIKI, KAFUNGA MABAO 801

 


Mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Manchester United Cristiano Ronaldo ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufikisha idadi ya mabao 800 kwenye michezo rasmi kwa ngazi ya klabu na timu ya taifa.


Ronaldo amefikia rekodi hiyo baada ya kufunga mabao mawili kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Arsenal, mchezo ambao Manchester United iliibuka na ushindi wa mabao 3-2. Mabao hayo mawili yamemfanya Ronaldo kufikisha mabao 801 na kuwa mchezaji wa kwanza kufanya hivyo katika historia ya mchezo huu pendwa.


Mchezaji huyo bora wa Dunia mara 5 amefunga idadai hiyo ya mabao akiwa na vilabu vinne tofauti pamoja na timu ya taifa ya Ureno. Katika mabao hayo amefunga mabao 130 akiwa na Manchester United ya England, mabao 450 akiwa na Real Madrid ya Hispania, mabao 101 akiwa na Juventes ya Italia na ameifungia timu yake ya taifa ya Ureno mabao 115.


Ronaldo mwenye umri wa miaka 36 msimu huu wa 2021-22 unaoendelea kwenye mashindano yote amefunga mabao 12 katika michezo 16 na mabao 6 kati ya hayo ni ya Ligi Kuu England (EPL).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.