ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 13, 2021

SIMBA YATHIBITISHA CHAMA KUONDOKA.

 


Kaimu Afisa habari wa Simba SC Ezekiel Kamwaga amethibitisha kuwa Kiungo wa kimataifa wa Zambia Cloutous Chama (30) amejiunga na Club ya RS Berkane ya Morocco akisaini mkataba wa miaka mitatu.

Chama amesaini mkataba huo unaotajwa kuwa umeigharimu RS Berkane ada ya uhamisho ya Tsh Bilioni 1.5 kwenda Simba SC na kuongezewa mshahara mara nne ya aliokuwa analipwa Simba SC.

Chama ambae ameonekana kwenye mazoezi ya RS Berkane akiwa na Tuisila Kisinda wa Yanga, alijiunga na Simba SC mwaka 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya Zambia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.