ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 13, 2021

GARI LAKWAMISHA MBOWE KUPELEKWA MAHAKAMANI

 


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu, wameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa kile kilichoelezwa ni changamoto ya usafiri wa gari la magereza.

Mbowe na wenzake wanakabiliwa na mashtaka sita yakiweno ya kufadhili vitendo vya ugaidi na kukusanya pesa kwa ajili ya kufanya vitendo vya kigaidi, katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 63/2020.

Mashtaka mengine ni kula njama za kutenda makosa, kukutwa na silaha aina ya bastola, risasi pamoja na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kinyume cha sheria.

Mbali na Mbowe, ambaye ni mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, wengine ni Halfan Hassan, Adam Kasekwa na Mohamed Lingwenya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.