ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 14, 2021

MBARONI KWA UHALIFU WA UTEKAJI, UBAKAJI NA KULAWITI WATOTO.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Mark Njera.

 


Jeshi la polisi Mkoani Mtwara limemkamata Jabiri Bakari  kwa kosa la kujihusisha na uhalifu wa utekaji, ubakaji na kulawiti watoto wa kike wenye umri chini ya miaka kumi katika wilaya ya Mtwara.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Mark Njera amewaambia waandishi wa habari leo kuwa mtuhumiwa huyo mwenye miaka 19 alikamatwa tarehe 12 August Mwaka huu  maeneo ya Mbae Manispaa ya Mtwara kufuatia msako wa jeshi la polisi uliofanywa.

Kamanda Njera amesema kabla ya kukamatwa na jeshi la polisi, mtuhumiwa aliwadanganya watoto wa kike watatu wenye umri wa miaka 8, 7 na mwingine mwenye miaka 9 ambao kwa nyakati tofauti aliwaiba sehemu mbalimbali kwa kuwalaghai kwa njia mbalimbali na kufanikiwa kuondoka nao kwenda kwenye maeneo na kuanzisha makazi ya mda akiwa na watoto hao.

Amesema mnamo tarehe 25 mwezi Juni mwaka huu mtuhumiwa alimlaghai mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 7 maeneo ya Mbae Mashariki wilaya ya Mtwara mtoto huyo akiwa anacheza na wenzake na baadae kuondoka naye ambapo mtoto huyo alipatikana baada ya siku tano akiwa amefanyiwa vitendo vya ukatili.

Mnamo tarehe 8 July maeneo ya Mbae, mtuhumiwa huyo alimchukua tena mtoto wa kike mwingine mwenye miaka 7 na kutoweka naye na kwenda kusikojulikana. Mtoto huyo alipatikana tarehe 24 Julya akiwa amefanyiwa vitendo vya kikatili.

Na mnamo tarehe 6 August mtuhumiwa huyo pia alimchukua mtoto mwenye umri wa miaka tisa ambaye pia alipelekwa kusikojulikana na mtuhumiwa huyohuyo na kufanyiwa vitendo vya ukatili. Kwa muhjibu wa kamanda Njera, mtoto huyo alipatikana tarehe 7 August kufuatia msako wa jeshi hilo.

Kamanda Njera ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mtwara kuhakikisha ulinzi na usalama kwa watoto na kutambua watu wanaojihusisha na vitendo vya ukatili kwa watoto na kutoa taarifa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.