ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 14, 2021

SIMBA YATAMBULISHA JEMBE LINGINE KUTOKA SENEGAL

 


RASMI kikosi cha Simba leo kimemtambulisha Pape Ousmane Sakho raia wa Senegal mwenye miaka 24.

Nyota huyo anakuwa ingizo jipya la nne ndani ya Simba baada ya jana Agosti 13 kumtambulisha Duncan Nyoni aliyeungana na Peter Banda pamoja na mzawa Yusuph Mhilu.

Nyota huyo anatajwa kuwa na uwezo mkubwa ndani ya uwanja pale anapopata nafasi akiwa ni kiungo mshambuliaji kinda aliyefanya vizuri kwenye ligi ya Senegal.  

Rekodi zinaonyesha kwamba alitupia mabao 8 na pasi 10 alitoa, pia ndiye mchezaji aliyeng'ara wakati timu ya Teungueth ikiitoa timu ya Raja Casablanca ya Morocco msimu ulioisha na kufuzu hatua ya makundi ya Caf Champions League.

Kwenye kambi nchini Morocco ambapo Simba wapo kwa sasa atajumuishwa na wengine ili kuendelea na maandalizi ya msimu ujao wa 2021/22.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.